Search This Blog
Thursday, May 23, 2019
Serikali kufanya ukaguzi miradi ya maji
Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa amesema serikali inaendelea kufanya ukaguzi wa kina wa miradi mbalimbali ya maji nchini ili kubaini utekelezaji wake kama umefanyika katika viwango vilivyokusudiwa na ile ambayo itakuwa imefanyika chini ya kiwango waliohusika watawajibishwa.
Mh Majaliwa ameyasema hayo bungeni leo wakati akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa waziri mkuu.
Kiongozi huyo akaongeza kuwa ni kweli ipo miradi mingi ya maji na utekelezaji wake umekuwa wa kusuasua na ndio maana kuna hatua mbalimbali ambazo mpaka sasa hivi zimechuliwa ili kukabiliana na changamoto zilizoko katika miradi hiyo.
Aidha Mh Waziri mkuu ametolea ufafanuzi masuala mengine ikiwemo kilimo na migogoro ya ardhi na hatua tofauti tofauti ambazo zimechuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa ili kuweka mambo sawa.
http://bit.ly/2JYriFv
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment