Search This Blog

Thursday, May 30, 2019

Raia wa Ufaransa ahukumiwa kifo Iraq kwa kujiunga na IS


Mahakama ya mjini Baghdad nchini Iraq imemhukumu kifo raia mmoja wa Ufaransa leo kwa kujiunga na kundi la itikadi kali linalojiita dola la kiisalamu.

Hatua hiyo imeifanya idadi ya wapiganaji wa jihadi ambao ni raia wa ufaransa wanaokabiliwa na hukumu ya kifo kuwa saba.

Yassin Sakkam alikuwa miongoni mwa raia 12 wa Ufaransa waliokabidhiwa kwa mamlaka za Iraqi mwezi Januari na vikosi vya Marekani vinavyopambana na kundi hilo la kigaidi nchini Syria.

 Sakkam amekiri mbele ya mahakama kula kiapo cha kulitumikia kundi la IS akisema alikuwa akipokea kila mwezi dola 70.

Sakkam ambae ana umri wa miaka 29 amesema mahakamani kwamba anajutia uamuzi wake wa kujiunga na kundi hilo na ameomba kusamehewa.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...