Search This Blog

Monday, May 27, 2019

Nina imani na kiongozi wa Korea Kaskazini - Rais Trump


Rais Donald Trump wa Marekani amesema kuwa ana imani na kiongozi wa Korea Kaskazini licha ya majaribio ya silaha yaliyofanywa hivi karibuni pamoja na kukwama kwa mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia.

Trump ambaye yuko Japan kwa ziara inayolenga kuimarisha mahusiano na mshirika huyo muhimu wa Marekani, amesema hivi leo kuwa majaribio ya silaha nchini Korea Kaskazini yaliyofanywa mapema mwezi Mei siyo jambo linalomtia wasiwasi. Matamshi ya Trump yanatofautiana na ya mshauri wake wa masuala ya usalama, John Bolton, ambaye hapo jana aliwaambia waandishi wa habari kuwa Korea Kaskazini imekiuka maazimio ya Umoja wa Mataifa kwa kufanya majaribio ya silaha.

Lakini katika ukarasa wake wa Twitter, Rais Trump ameandika kuwa ana matumaini Kim Jong Un ataheshimu ahadi aliyoitoa kuhusu suala la majaribio ya silaha. Korea Kaskazini ni moja ya masuala muhimu ya majadiliano wakati Trump atakapokutana na Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe.

http://bit.ly/2HVLlSp

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...