Search This Blog
Wednesday, May 29, 2019
Naibu spika aichangia Klabu ya Yanga
Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dk Tulia Ackson ametoa Sh. milioni moja kwa ajili ya kuichangia Klabu ya mpira wa miguu ya Yanga huku akitoa wito kwa Watanzania kujitokeza kwa kuichangia timu hiyo.
Dk Tulia ametoa mchango huo leo, Ofisini kwake bungeni jijini Dodoma kwa kuukabidhi kwa viongozi ambao ni wabunge wapenzi wa Yanga wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya kuhamasisha michango ya timu hiyo, Anthony Mavunde.
Wabunge wengine waliokuwepo katika kupokea mchango huo ambao ni wapenzi wa Yanga ni Hawa Ghasia (Mtwara Vijijini-CCM), Vanance Mwamoto (Kilolo-CCM), Mohamed Mchengerwa (Rufiji-CCM) na Mussa Ntimizi (Igalula-CCM).
Akizungumza kabla ya kukabidhi mchango huo, Dk.Tulia amesema aliahidi kuichangia timu hiyo na sasa anatimiza ahadi yake.
“Niliahidi kuchangia Yanga na nimekabidhi Sh. milioni moja na ninawaomba sana Watanzania kuwachangia Yanga kwani wanahitaji sana michango.”amesema Dk Tulia.
Aidha ametoa wito kwa Watanzania kujitokeza Juni 15, 2019 katika shughuli iliyoandaliwa na Yanga ambayo imepewa jina la ‘Kubwa Kuliko’ itakayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment