Search This Blog

Monday, May 27, 2019

Kijana mbaroni kwa kumpiga mpenzi wa mama yake


Kijana David Omondi(20) anadaiwa kumpiga na kumsababishia majeraha mwanaume anayesemekana kuwa ni mpenzi wa mama yake huko Sinapanga katika Kaunti ya Bondo nchini Kenya.

Mwenyekiti wa Polisi jamii wa Kaunti hiyo, Juma Abuko amesema mtuhumiwa alimfuata mwanaume huyo anayedaiwa kuwa kwenye uhusiano na mama yake na kumtaka amueleze kwanini ameingia kwenye mahusiano na mamake huku akijua kuwa ameolewa.

Kabla hajapewa majibu ya maswali yake, David alianza kumshambulia kwa kipigo mwanaume huyo na ndipo watu walipoenda kuamua ugomvi na kumpeleka majeruhi hospitali huku David akipelekwa kutuo cha Polisi anaposhikiliwa hadi sasa.

http://bit.ly/2JFNnJV

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...