Search This Blog
Tuesday, May 28, 2019
Jimbo la Kubenea, Mnyika 2020 lazima yarudi CCM - Mavunde
Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Antony Mavunde amesema mwaka 2020 ni lazima majimbo mawili Ubungo na Kibamba yarudi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Jimbo la Ubungo likiwa nila Kubenea na Kibamba likiwa ni la Mnyika, yote haya yakiwa yanaongozwa na chama Upinzani (Chadema).
Akizungumza kwenye kampeni maalum inayoendeshwa na Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) amesema CCM itahakikisha Dar es salaam inakuwa ya kijani kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu.
“Kama kuna uhitaji wa maji, barabara nzuri vyote vinafanyika sasa kuna haja gani ya kubakia upande wa pili wa upinzani ni lazima vijana kufanya kazi kuhakikisha majimbo yanarudi CCM na katika uchaguzi wa serikali za mitaa kata zote ziwe chini ya chama chetu.
“Jitahidini viongozi hii ni aibu anzeni na mitaa yote 91 kuhakikisha inarudi ndani ya CCM maana nikiangalia hapa hakuna kupita Mnyika wala Kubenea watapitia wapi?,’’amesema Mavunde.
Aidha Waziri huyo amesema makosa yalifanyika hapo awali yakuachia majimbo hayo kuchukuliwa na chama cha upinzani chini ya Mbunge, John Mnyika (Kibamba ) na Mbunge, Saed Kubenea (Ubungo), hayatafanyika tena kwa kuwa hakuna wanachokifanya zaidi ya kutekeleza ilani ya CCM.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment