Search This Blog

Saturday, May 25, 2019

Dereva aliyemgonga Twiga Mikumi kupigwa faini Milioni 34


Dereva ambaye jina lake halijajulikana anayedaiwa kumgonga na kumuua mnyama Twiga katika mbuga ya wanyama ya Mikumi, Mkoani Morogoro amekimbia baada ya kufanya tukio hilo.

Anasteria Ndaga, Afisa Uhifadhi Wanyama Pori Kanda Ya Mashariki amesema mnyama huyo aligongwa jana saa tano asubuhi, ambapo wanalishikilia gari hilo pamoja na msaidizi wa dereva wa gari hilo na amefikishwa katika kituo cha polisi.

‘’Dereva wa gari hilo amekimbia na hajapatikana hadi leo, tunawasiliana na mmiliki wa gari ili taratibu zingine zitafuata za kisheria’’ amesema.

Ameendelea kwa kusema, "Sheria za Uhifadhi za Taifa, zinasema mnyama kama Twiga anapogongwa faini ni U$ Dollar elfu 15, sawa na Mill. 34 za Kitanzania, pia zipo gharama zingine za uharibifu wa mazingira, hatujampima kama alikuwa mjamzito’’.

http://bit.ly/2QmtUyp

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...