Search This Blog

Tuesday, May 28, 2019

Ajeruhi watu 17 kwa kuwachoma na visu


Watu wawili akiwemo mtoto mmoja wanahofiwa kupoteza maisha huku wengine 17 wakijeruhiwa katika shambulio kubwa la uchomaji visu katika mji wa Kawasaki nchini Japan.

 Maafisa wa zimamoto wanasema, tukio hilo limetokea majira ya asubuhi hii leo, ambapo mwanaume mmoja aliwashambulia watu kwa kuwachoma visu.

 Kwa mujibu wa mashuhuda mshambuliaji aliwalenga wanafunzi katika kituo cha basi. Polisi wanasema mshukiwa tayari amekamatwa, na ripoti za shirika la habari la Japam NHK, ni kwamba mshambuliaji huyo pia alijichoma visu na alikuwa na majereha makubwa.

Japan ni nchi iliyo na viwango vya chini vya uhalifu na mashambulizi makubwa yamekuwa nadra sana. Mwaka 2018 mwanaume mmoja alikamatwa baada ya kumshambulia kwa kisu na kumuua mtu mmoja huku wengine wawili wakijeruhiwa ndani ya treni. Tukio hilo lilichochea hatua za usalama kuimarishwa.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...