
Wanajeshi wa serikali ya Ethiopia wanatumwa kuelekea mstari wa mbele wa mzozo na waasi wa Tigraya, mashahidi kaskazini mwa Ethiopia wameambia BBC.
Mwandishi wa kituo cha redio cha Marekan NPR katika mji wa Kombolcha, alisema wanajeshi hao walikuwa wameandamana na wanamgambo washirika wa serikali wakiwa na silaha zilizoboreshwa zikiwemo mapanga, mashoka na majembe.
Walisema wanahofia kuuawa na Watigray ikiwa watashindwa kusitisha hatua hiyo.
BBC haijafanikiwa kuthibitisha madai hayo.
Mji wa Kombolcha umefurika wakazi wanaotorokamaeneo ya Tigray yanayoshikiliwa, baadhi ya maeneo hayo kulingana na Umoja wa Mataifa yanakabiliwa hali ya njaa baada ya serikali kuyafungia.
Msemaji Watigray amesema kuwa waasi wanaendelea kukabiliana na maadui, lakini bado wako mbali na Kombolcha.
No comments:
Post a Comment