Search This Blog

Saturday, October 2, 2021

Waandishi wa habari wanawake,Njombe wanogesha maadhimisho ya siku ya wazee Duniani


Na Amiri Kilagalila,Njombe

Katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya wazee duniani waandishi wa habari wanawake mkoani Njombe wamepongezwa kwa kuandaa hafla fupi  iliyowakutanisha baadhi ya wazee na kusheherekea nao pamoja na kuhamasisha zoezi la chanjo ya Uviko 19

Akizungumza kwenye halfa hiyo ambayo imefanyika katika ukumbi wa Turbo mjini Njombe mgeni wa heshima ambaye ni mwenyekiti wa jumuiya ya umoja wa wanawake wa Chama cha Mapinduzi (UWT) wilaya ya Njombe Beatrice Malekela amesema jamii inatakiwa kuwakumbuka wazee kwa kuwasaidia mahitaji muhimu kama ambavyo kundi la wanahabari wanawake mkoa wa Njombe lilivyofanya.

"Pia serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania imeweza kuwatambua wazee wa mikoa yote ambapo kwa mkoa wa Njombe tuna wazee 39,768 na kwa kweli niwapongeze sana waandishi wa habari kwa hiki mlichokifanya kwani mmeiunga mkono serikali katika juhudi za kuwasaidia wazee"alisema Betrice Malekela

Aidha Betrice amesema serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inathamini uwepo wa wazee kwenye jamii ambapo imewapa kipaumbele katika kupata za huduma za afya kwa kuwapatia vitambulisho vinavyowasaidia kupata matibabu bure.


Sophia Issa ni mwenyekiti wa muda wa umoja wa waandishi wa habari wanawake mkoa wa Njombe amesema watahakikisha wanaendelea kuandika habari zenye kuwakumbusha watanzania wafahamu umuhimu wa wazee na kuondoa dhana potofu juu yao.

"Wanahabari tumekuwa tukifanya kazi nyingi huko vijijini zinazohusu wazee na changamoto zao ikiwemo za kutelekezwa.Tunaendelea kuhamasisha watoto walioenda mijini na kuwaacha wazee vijijini waweze kuwakumbuka wazazi,babu na bibi zao" alisema Sophia Issa

Kwa upande wa baadhi ya wazee waliohudhuria hafla hiyo wamewashukuru wanahabari wanawake kwa kuwajali huku pia wakiowaomba baadhi ya vijana wawakumbuke wazee na kuwatunza.

"Kwa serikali tunashukuru kwa huduma ya afya,Mimi mwenyewe natibiwa bure na pia niwaombe vijana wasitunyanyapae sisi wazee"alisema mmoja wa wazee

Waandishi hao wanawake wa mkoa wa Njombe wamekabidhi zawadi mbali mbali kwa wazee ikiwemo Sukari,sabuni na mafuta ya kupikia

Maadhimisho ya siku ya kimataifa ya wazee Duniani yanayoadhimishwa leo Octoba 1,2021 yameambatana na kauli mbiu isemayo "Matumizi sahihi ya kidigitali kwa ustawi wa rika zote".


 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...