
Vijana wadogo waliokuwa na kukamatwa na polisi miezi kadhaa iliyopita na kupelekwa katika jimbo la Katanga sasa wanapambana na njaa.
Vijana hap walipelekwa Katanga miezi kadhaa iliyopita chini ya mpango wa Huduma kwa taifa- tawi maalum la jeshi la DRC linalofanya kazi ofisi ya rais .
Vijana hao wamekuwa wakifanya shughuli mbali mbali za kilimo na Alhamis wiki hii, waliweza kuvuna mavuno yao ya kwanza na kuyauza kwa kiwango cha chini katika mjini Kinshasa.Awali baadhi ya mashirika ya yasiyo ya kiserikali (NGO) yalilaani hatua ya polisi ya kuwakamata magenge ya vijana mwezi Novemba mwaka jana. Kamanda wa kikosi cha Huduma kwa taifa Meja Jenerali Jean Pierre Kasongo alisema kuwa kuna mipango ya kuwaajiri vijana hao kama wahudumu wa umma
No comments:
Post a Comment