Search This Blog

Tuesday, October 19, 2021

Uganda yazindua gari la kivita lililoundwa nchini humo

 


Kamanda wa vikosi vya ardhi nchini Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, ameweka kwenye Twitter picha ya kile anachosema kuwa gari la kwanza la kivita kutengenezwa nchini humo.


Anasema "liliundwa na kutengenezwa ncini Uganda", lakini hakutoa maelezo kuhusu muundo na gharama yake.


Gari hilo lililopewa jina la Chui - lilizinduliwa na baba yake, Rais Yoweri Museveni.


Jeshi la Uganda mwaka jana lilihusika katika msako mkali dhidi ya maandamano yaliyotikisa mji mkuu, Kampala, kufuatia kukamatwa kwa mgombea urais Bobi Wine.


Maafisa walitete utumizi wa silaha za moto, wakisema polisi na jeshi walikua wakikabiliana na waandamanaji.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...