Search This Blog

Friday, October 22, 2021

Nyota wa sinema Alec Baldwin amuua mwanamke kutumia bunduki wakati wa kutengezwa filamu yake

Mwanamke amekufa na mwanaume amejeruhiwa baada ya muigizaji Alec Baldwin kufyatua risasi kutumia bunduki ya maigizo kwenye seti ya filamu huko New Mexico.

Polisi katika jimbo hilo la Marekani walisema Bw. Baldwin alitoa silaha hiyo wakati wa utengezaji wa filamu yake

Mwanamke huyo alipelekwa hospitalini lakini alifariki kutokana na majeraha yake. Mwanaume aliyejeruhiwa -mkurugenzi wa filamu, alikuwa akipokea huduma ya dharura.

Msemaji wa Bw Baldwin aliliambia shirika la habari la AP kwamba kisa hicho kilihusisha utumiaji mbaya wa bunduki ya maigizo.

Mwanamke huyo ametajwa kama Halyna Hutchins, 42, ambaye alikuwa akifanya kazi kama mkurugenzi wa upigaji picha. Mtu anayetibiwa ni Joel Souza, 48, mkurugenzi wa filamu.

Polisi bado wanachunguza tukio hilo huko Bonanza Creek Ranch, eneo maarufu la utengenezaji wa sinema, na hakuna mashtaka yoyote yaliyofunguliwa.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...