Search This Blog
Monday, October 11, 2021
Naombeni mnisaidie nimeteseka zaidi ya miaka 10- Felista
Na Maridhia Ngemela,Mwanza
Nimelala hapa kitandani zaidi ya miaka 10 nakutegemea familia yangu inihudumie kila kitu naiomba Serikali inisaidie nateseka na huu ugonjwa.
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameombwa kutoa msaada wa hali na mali ili kuweza kunusulu maisha ya Felista Edward ambaye ni mgonjwa kwa zaidi ya miaka 10 akiwaamelala kitandani bila kuamuka kwa sababu ya kusumbuliwa na bandama na kupelekea tumbo kuvimba na miguu.
Mgonjwa huyo ambaye ni mkazi wa mtaa wa mchongomani uliyopo wilayani Ilemela Mkoani Mwanza alisema amelala kitandani zaidi ya 10 kwa sababu ya kuugua ugonjwa huo.
"Tangu nilipoanza kuugua ugonjwa huu ninamiaka 21 ila nilikuwa sijazidiwa hivi lakini ninamiaka zaidi ya 10 nipo kitandani siwezi kifanya kitu chochote na nimetibiwa hospitali ya rufaa ya mkoa ya Sekou toure lakini sasa hivi sina fedha ya matibabu zaidi ya kununua vidonge kwenye maduka tu.
"Nimevimba kuvimba tumbo na miguu na siwezi hata kukaa wala kujigeuza naomba wananchi na viongozi mbalimbali waweze kunisaidia fedha za matibabu ili niweze kwenda kutibiwa kwenye hospitali kubwa kama mnavyoniona hapa nateseka hakuna kitu kinaumiza kama kumtegemea kufanyiwa kila kitu.",alisema Felista.
Naye Kassimu Masota ambaye ni mume wa mgonjwa huyo alisema kwa hivi sasa hawezi kufanya kazi yoyote zaidi ya kumuuguza mke wake jambo ambalo linapelekea familia kukosa kipato cha kujikimu kimaisha.
"Naomba msaada wa hali na mali kwa jamii na serikali ili niweze kumtibu mke wangu ambaye amelala kitandani zaidi ya miaka 10 bila kupata nafuu kwa hivi sasa hawezi kukaa wala kutembea na tumbo na miguu vimevimba.
"Kupitia kuuguliwa na mke wangu nina mtihani mkubwa kwani uwezo wa kununua chakula, maji sina na vyote vinahitajika na hivi sasa sifanyi kazi yoyote zaidi ya kuuguza nawaombeni msaada wenu,"alisema Masota.
Mwalimu Tatu Ngelangela ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi Kilimahewa alisema baada ya kutomuona mwanafunzi wake shuleni hapo kwa mda mrefu ndipo alipofatilia na kubaini tatizo hilo.
"Nilipoona mwanafunzi wangu haji shuleni nilimfatilia na kubaini anaishi na bibi yake ambaye anatatizo hili nilichukua jukumu la kuwaita waandishi ili waweze kumsaidia apate msaada wa matibabu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment