
Msanii maarufu wa Ghana ambaye alisema amekimbilia mafichoni kwa kuhofia usalama wake amejisalimisha, polisi inasema.
Watu wengine wawili pia wamekamatwa kwa "kueneza taarifa za uwongo" juu ya shambulio la bunduki dhidi ya Shatta Wale.
"Amekamatwa ili kusaidia polisi katika uchunguzi wa madai yake ya kuhusika katika uundaji na usambazaji wa habari inayokusudiwa kusababisha hofu na taharuki, "polisi walisema juu ya kukamatwa kwa mwanamuziki huyo.
Polisi walitanga kukamatwa kwake Jumanne sa kadhaa baada ya msanii huyo kuweka ujumbe mtandaoni akisema "maisha yake yako hatari"
No comments:
Post a Comment