Search This Blog

Wednesday, October 13, 2021

Mdogo wa rais wa zamani wa Algeria afungwa


Mdogo wa aliyekuwa rais wa Algeria hayati, Abdelaziz Bouteflika, amefungwa gerezani kwa kipindi cha miaka miwili kwa kosa la kukwamisha haki kutendeka.

Said Bouteflika alifungwa pamoja na waziri wa zamani wa haki, Tayeb Louh, pamoja na mfanyabiashara , Ali Haddad.

Bwana Louh atatumikia kifungo cha miaka sita wakati bwana Haddad atafungwa miaka miwili.

Wote watatu walikamatwa baada ya rais Bouteflika alipoondolewa madarakani kwa lazima mnamo mwaka 2019.

Rais wa zamani wa Algeria ,Bouteflika alifariki mwezi uliopita, miaka nane baada ya kuugua kwa muda mrefu.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...