Bustani nzuri ili iweze kuzalisha kitu ambacho ni kizuri inategemeana sana na jinsi mmiliki wa bustani hiyo jinsi anavyoihudumua. Kama hutawekeza juhudi za kutosha katika kuhakikisha bustani inakuwa vizuri muda wote ni kwamba mimea ya bustani hiyo ni lazima itakufa tu hata iwaje.
Kama ilivyo kwenye bustani hata mahusiano yenu yanaweza kuwa mazuri yenye kuwapa tulizo au mabaya kuendana na kujitoa kwenu kuyatunza na kupambana na changamoto zozote zile kwenye vipindi vya shida na raha.
Ndani ya mahusiano kuna chanagamoto nyingi sana ambapo kimsingi kama wahusika hawatakuwa makini na yale wanayoyasikia na kuyaona ni kwamba mahusiano yao hayatafika mbali sana.
Watu wataleta choko choko za kuwagombanisha kama mhusika fulani hata kuwa makini kwamba mtu anaweza kujikuta anamuacha yule ampendaye pasiyo kufanya uchunguzi wa kutosha juu wa yale aliyoyasikia.
Asikwambie mtu wangu wa nguvu, Inachosha sana pindi we unahangaika kuyapalilia, kumwagilia mahusiano yako ya kimapenzi ili yastawi, halafu watu wengine wanakuja kwa kasi kubwa kwa ajili ya kung'oa mazao badala ya magugu. Inauma sana.
Hivyo ni wajibu wako kuanzia sasa kujua namna sahihi ya kuitunza bustani yenu ya mahusiano ya kimapenzi ili mahusino yenu yaweze kudumu daiama, Ni wajibu wenu kuhakikisha mnalinda mahusiano yenu kila itwapo leo,
Na; Benson Chonya.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment