Search This Blog

Tuesday, October 19, 2021

Afrika yahitaji dola bilioni 50 kwa mwaka kupambana na mabadiliko ya tabia nchi

Ripoti mpya inasema Afrika inahitaji kuwekeza $50bn (£36bn) kwa mwaka ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Umoja wa Afrika na taasisi ya hali ya hewa duniani imeonya kuwa watu maskini wapatao milioni 120 wanakabiliana na mafuriko, ukame, kuhama makazi yao na joto lililopita kiasi ifikapo mwishoni mwa muongo kama hakuna jitihada zitafanyika.

Vilevile wameonya juu ya barafu zote zilizopo barani Afrika kuwa ziko njiani kutoweka ifikapo miaka ya 2040.

Afrika imepata joto haraka kuliko wastani wa ulimwengu ingawa imewajibika kwa 4% tu ya uzalishaji wa hewa chafu duniani.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...