Ripoti mpya inasema Afrika inahitaji kuwekeza $50bn (£36bn) kwa mwaka ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Umoja wa Afrika na taasisi ya hali ya hewa duniani imeonya kuwa watu maskini wapatao milioni 120 wanakabiliana na mafuriko, ukame, kuhama makazi yao na joto lililopita kiasi ifikapo mwishoni mwa muongo kama hakuna jitihada zitafanyika.
Vilevile wameonya juu ya barafu zote zilizopo barani Afrika kuwa ziko njiani kutoweka ifikapo miaka ya 2040.
Afrika imepata joto haraka kuliko wastani wa ulimwengu ingawa imewajibika kwa 4% tu ya uzalishaji wa hewa chafu duniani.
No comments:
Post a Comment