
Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergey Lavrov alisema kuwa kuna fursa za utatuzi wa amani wa suala la Afghanistan,
"Natumai mazungumzo yataanza tena kati ya Taliban na vikundi vya Tajik vya Afghanistan," alitoa maelezo hayo.
Lavrov alitoa taarifa juu ya maswala ya hivi karibuni katika mji mkuu wa Moscow.
Akitathmini suala la Afghanistan, Lavrov alisema kuwa mazungumzo kati ya vikundi vya Tajik katika mkoa wa Panjshir na Afghanistan na Taliban yamesitishwa.
Lavrov alisema,
"Kuna fursa za utatuzi wa amani wa suala la Afghanistan. Natumai kuwa cheche za makabiliano ya mwisho katika Bonde la Panjshir kaskazini mwa Afghanistan zitageuka kuwa mazungumzo ya upatanishi. Mazungumzo haya yalikuwa yameanza, kisha yakaingiliwa na mapigano yakaanza. Natumai mazungumzo kati ya Taliban na vikundi vya Tajik vya Afghanistan yataanza tena. "
Akifahamisha kuwa wanawasiliana na vikosi vyote vya kisiasa na vya kikabila nchini Afghanistan, pamoja na Taliban, Lavrov alisema kuwa wamechukua hatua za kuanzisha mazungumzo kati ya vikosi hivi.
Lavrov aliongezea kusema kuwa,
"Suluhisho la kisiasa lazima lijumuishe upatanisho kati ya jamii za Wapashtun, Tajik, Uzbek, Hazara zinazowakilishwa na Taliban."
No comments:
Post a Comment