Search This Blog

Thursday, September 2, 2021

Watendaji wa Kata 16 Same wakabidhiwa pikipiki



Halmashauri ya wilaya ya
Same mkoani Kilimanjaro imetumia shilingi milioni 37.6 zilizobaki baada ya kununua gari la Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, kununua pikipiki 16 kwa ajili ya watendaji wa kata ili waweze kuzitumia kukusanya mapato.

Akizungumzia hatua hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Same, Annastazia Tutuba amesema katika mwaka wa fedha wa 2020/2021 walipokea kutoka hazina shilingi milioni 210, ambapo walinunua gari la Mkurugenzi kwa shilingi milioni 162.

Amesema baada ya fedha kubaki, waliomba kibali hazina cha kununua pikipiki hizo, ili Watendaji wa kata hasa zilizoko milimani ambapo kuna changamoto ya usafiri waweze kuzitumia kukusanya mapato ya Serikali bila usumbufu.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...