Search This Blog

Thursday, September 2, 2021

Wanafunzi wengine 73 watekwa Nigeria


Wanafunzi 73 wametekwa nyara na watu wenye silaha katika shule ya sekondari ya kaskazini magharibi mwa Nigeria.
 
 Kulingana na taarifa rasmi ya polisi, Kundi la watu wenye silaha lilivamia shule hiyo ya eneo la Kaya katika mkoa wa Maradun la Jimbo la Zamfara mapema jana asubuhi, na kuwateka nyara wanafunzi hao. 
 
Timu za uokozi za polisi zinafanya kazi pamoja na wanajeshi kujaribu kuwakomboa wanafunzi hao, amesema msemaji wa polisi Mohammed Shehu. Utekaji nyara wa wanafunzi umekuwa ni jambo lilozoeleka kaskazini magharibi na katikati mwa Nigeria. 
 
Karibu wanafunzi 1,000 walitekwa mwaka huu - na baadae wengi wao waliachiliwa. Rais Muhammadu Buhari yuko chini ya shinikizo kutokana na nchi yake kukosa usalama. 
 
Licha ya juhudi za wanjeshi za kupambana na wahalifu hao, mashambulizi na utekaji nyara bado yanaendelea.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...