Search This Blog

Wednesday, September 1, 2021

Tetesi za soka kimataifa


Real Madrid haikufanikiwa na ofa yao mpya ya euro milioni 220 (pauni milioni 189) kwa mshambuliaji wa Paris St-Germain Kylian Mbappe, 22. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa sasa atakuwa huru kujadili mkataba wa mapema na kilabu hicho cha Uhispania mnamo Januari kabla ya kujiunga nao kwenye uhamisho wa bure msimu ujao. (Goal)

Mshambuliaji wa Manchester United na Ufaransa Mfaransa Anthony Martial, 25, amekataa nafasi ya kujiunga na Lyon katika dakika ya mwisho siku ya mwisho ya usajili.(L'Equipe, via Mirror)

Tofauti na Martial, kiungo wa kati wa United Donny van de Beek, 24, alitaka kuondoka Old Trafford - lakini Ole Gunnar Solskjaer akazuia uhamisho wa mkopo wa Mholanzi huyo kwenda Everton. (AD - in Dutch)

Atletico Madrid imekataa dau la pauni milioni 18 kwa beki wa kulia wa England Kieran Trippier, 30, kutoka Manchester United, na kuchochea kilabu hicho cha Ligi Kuu ya Primia kumzuia mlinzi huyo wa Ureno mwenye umri wa miaka 22 Diogo Dalot kuhamia Borussia Dortmund. (Sport1, via Star)

Tottenham haikurudi na mkataba bora kwa winga Adam Traore baada ya kukataliwa ofa yao ya pauni milioni 30 Jumatatu. Wolves alidai pauni milioni 50 kwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania mwenye umri wa miaka 25. (Athletic)

Wolves iliendelea na juhudi zake za kumsaka kiungo wa kati wa Marseille na Ufaransa Boubacar Kamara, 21, wa Under-21, baada ya jaribio la kumsajili Renato Sanches wa Ureno, 24, kutoka Lille. (Athletic - subscription required)

West Ham walikuwa na hamu ya kumsajili kiungo wa kati wa England Jesse Lingard, 28, kutoka Manchester United kufuatia mafanikio yake katika makubaliano ya mkopo msimu uliopita, lakini haikuwa tayari kufikia bei ya kilabu ya Old Trafford ya pauni milioni 25. (Talksport)

Newcastle ilishindwa na jaribio lao la kumsajili kiungo wa zamani wa England wa Under-21, Hamza Choudhury, 23, kutoka Leicester baada ya majadiliano kati ya vilabu hivyo viwili kuvunjika. (Sky Sports)

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...