Taiwan imesema uvamizi mkubwa wa ndege za jeshi la China ziliruka katika eneo lake la ulinzi wa angani Jumapili.
Wizara ya ulinzi ilisema ndege 19 pamoja na ndege za kufanya mashambulio zenye uwezo wa nyuklia ziliingia katika eneo la ‘utambulisho wa ulinzi wa anga (ADIZ).
Taipei imekuwa ikilalamika kwa zaidi ya mwaka mmoja juu ya misheni zinazofanywa kila mara na jeshi la anga la China karibu na kisiwa hicho.
China inaiona Taiwan yenye demokrasia kama jimbo lake lililojitenga, lakini Taiwan inajiona kama nchi huru.
Wizara ya ulinzi ya Taiwan ilisema ndege hizo za China zilisheheninne za kurusha mabomu za H-6 ambazo zinaweza kubeba silaha za nyuklia pamoja na ndege za kushambulia manowari.

No comments:
Post a Comment