Uongozi wa Klabu ya Simba umepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za kifo cha Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi, Zacharia HansPope ambaye amefariki dunia.
Hanspope ambaye alikuwa ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ndani ya Simba alikuwa anaumwa na taarifa zake za kutangulia mbele za haki imetolewa usiku wa kuamkia leo.
Miongoni mwa waliomlilia ni pamoja na Haji Manara, Ofisa Habari wa Simba, Emmanuel Okwi nyota wa zamani wa Simba pamoja na viongozi mbalimbali wa Simba ambao wamesema kuwa wameshtushwa na taarifa hiyo.

No comments:
Post a Comment