Search This Blog

Sunday, September 26, 2021

Silinde atoa maagizo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri nchini

 


Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. David Silinde amewaagiza wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanasimamia  nidhamu ya watumishi  waliochini ya  kwa kuhakikisha wanatenda haki  na kufuata miongozo kanuni na sheria  za utumishi wa umma.

Akifunga Mafunzo ya wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa leo Jijini Dodoma Mhe. Silinde amesema amewataka kuhakikisha wanazingatia mipaka ya madaraka  na hatua zinazochukuliwa dhidi ya watumishi zifuate  sheria, kanuni  na taratibu  za utendai  kazi katika utumishi wa umma na Serikali kwa ujumla.

Mhe. Silinde  amesema ni wajibu wa wakurugenzi kuhakikisha wanatatua kero za wananchi ameaagiza wakurugenzi hao kutatua kero za wananchi  hasa walioko maeneo ya vijijini  ambao wengi ni masikini  kwa kuhakikisha wanapatikana kirahisi maofisini na kuondoa urasimu  usio wa lazima.

Ameendelea kufafanua kuwa bado kuna maeneo fedha za Serikali zinapotea na kuingia katika mifuko ya wajanja kwa kutumia risiti za mikono, amewataka kuhakikisha wanatumia mifumo ya kielektroniki katika ukusanyaji wa mapato

Vilevile, Amewagiza kuhakikisha wanasimamia  matumizi sahihi za fedha za Serikali  na zitumike kwa  malengo yaliyokusudiwa  na kulingana  na thamani  ya fedha zilizotumika ikilinganishwa na huduma  iliyotolewa.

Mhe. Silinde qmewataka kuhakikisha wanasimamia ubunifu na uhodari katika kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia mipango  ya wananchi kupitia Halmashauri zao, na kuhakikisha wanasimamia  utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri zao 

Aidha, Mhe. Silinde amesema ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi  vi vyema wakaongeza kasi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa, nyumba za waalimu , vituo vya afya, vituo vya maji safi na salama.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...