Search This Blog

Wednesday, September 29, 2021

Shambulio la angani la Nigeria lawaua raia karibu na ziwa Chad


Raia kadhaa wameuawa katika shambulio la angani la Nigeria lililokua likiwalenga washukiwa wa makundi ya kijihadi karibu na ziwa Chad, ambayo inapita kaskazini-mashariki mwa Nigeria na nchi tatu jirani.

Tukio hilo linakuja chini ya wiki mbili baada ya shambulio lingine dhidi ya kijiji kuwaua raia kaskazini -mashariki mwa Nigeria, ambako majeshi yanakabiliana na wanamgambo wa kijihadi.

Maelezo bado yanaibuka kutoka eneo la Kwantan Daban Masara, ambapo shambulio hilo lilifanyika Jumapili asubuhi.

Haijabainika ni raia wangapi waliuawa katika shambulio hilo, au ikiwa walikuwa na uhusiano na kundi la Wanamgambo Islamic State katika eneo la Afrika Magharibi (Iswap), ambalo linahudumu katika eneo hilo.

Shirika la Habari la AFP linasema karibu wavuvi 20 waliuawa. Shirika la Habari la Reuters liliwanukuu watu wawili- mkazi na mhasiriwa alijyeruhiwa- wakisema karibu watu 50waliuawa baada ya Jeshi la Anga la Nigeria kuwafyatulia risasi raia kadhaa.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...