Rais wa Iran Ebrahim Raisi amesema nchi yake iko wazi kuhusu shughuli zake za nyuklia. Kwa mujibu wa taarifa ya ofisi ya rais, kiongozi huyo amemfahamisha rais wa baraza la Ulaya Charles Michel kwa njia ya simu kwamba ushirikiano wa dhati wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na shirika la kimataifa la kudhibiti silaha za nyuklia IAEA ni mfano mzuri kwamba Iran inazingatia uwazi kuhusu shughuli zake za nyuklia.
hata hivyo shirika la IAEA lisema kazi yake ya usimamizi nchini Iran imekwama kwa kiwango kikubwa tangu Februari 23 baada ya serikali ya Iran kusitisha baadhi ya kazi zake za ukaguzi katika mpango wa nyuklia wa nchi hiyo.

No comments:
Post a Comment