
Kiungo wa kati wa klabu ya Manchester United Paul Pogba aliisaidia klabu yake kuilaza Newcastle4-1siku ya Jumamosikabla ya kujiunga na nyota wa muziki wa Nigeria Burna Boy kuwatumbuiza raia.
Pogba ambaye familia yake inatoka nchini Guinea , alicheza pamoja na Cristiano Ronaldokatika uwanja wa Old Trafford huku nyota huyo wa Ureno akifunga magoli mawili baada ya kurudi katika timu hiyo kutoka Juventus.
Mchezaji huyo ambaye ni mshindi mara mbili wa kombe la dunia na Ufaransa , alitoa pasi mbili za magoli kabla ya kwenda katika tamasha la muziki la Parklife music festival mjini Manchester na kushiriki pamoja na Burna Boy, ambaye alikuwa amevalia tishati ya Manchester United.
No comments:
Post a Comment