
Shirikala Afya Duniani linasema kuwa ni mataifa 14 pekee ya Afrika yamefikia lengo la kuchanja asilimia 10 ya raia wao dhidi ya Covid-19.
Hii ni kwa sababu mpango wa Covax, unaolenga kusaidia nchi masikini kupata chanjo haujafanikiwa kufanya hivyo baada ya nchi tajiri kununua chanjo zote.
Kati ya nchi hizo 14 ni Ushelisheli, Mauritius na Morocco ambazo zimefanikiwa kufikia lengo la kimataifa la chanjo dhidi ya Covi-19 kufikia sasa.
Asilimia 14 ya raia wa nchi hizo tatu wamepata chanjo kamili.
Nchi zinine zilizofikia lengo la kamataifa la chanjo hiyo ni Tunisia, Eswatini, Cape verde, Botswana, Comoros, Zimbabwe, Equatorial Guinea, Afrika Kusini, Mauritania, Lesotho na Rwanda.
Mpango wa chanjo wa Covax ulitarajiwa kuwasilisha dozi milioni 274 za chanjo kwa nchi za Afria kufikia mwisho wa mwezi Septemba, lakini imefanikiwa kuwasilisha zaidi ya dozi milioni tano.
No comments:
Post a Comment