Search This Blog

Thursday, September 9, 2021

Mlipuko wa ugonjwa wa uti wa mgongo wauwa 120, DRC


Mlipuko wa ugonjwa wa uti wa mgongo au meningitis umetangazwa kaskazini- mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Mpaka sasa watu zaidi ya 120 wamekufa kutokana na ugonjwa huo.

Mgonjwa wa kwanza nchini DRC aliripotiwa Julai.

Zaidi ya watu 100 wamepata tiba wakiwa nyumbani au vituo vya afya.

Mlipuko huo umekuwa mgumu kukabiliana nao kwa kuwa jamii inauhusisha na uchawi, shirika la afya duniani (WHO) limeiambia BBC.

Sampuli zilizotumwa Ufaransa zimebaini kuwa bakteria wanaohusika na mlipuko huo wanaweza kusababisha janga kubwa.

Watu wengi wamekufa na jamii inapaswa kulaumiwa kwa kushindwa kuwajibika.

Badala ya kutafuta tiba, baadhi ya watu wamekuwa wakitoka sehemu moja kwenda nyingine wakiwa na matumaini kuwa ugonjwa huo hautawafuata.

Serikali ya DRC na WHO wametuma vikosi vya watumishi wa afya kaskazini mashariki mwa jimbo la Tshopo ili kukabiliana na hali hiyo.

Baadhi yao hawana uwezo na wako katika hatari kwa milipuko ya mara kwa mara haswa wakati wa kiangazi - kutoka Januari hadi Julai.

Meningitis, ni ugonjwa ambao unaweza kusababisha kifo, unaambukiza kutoka kwa mtu mwenye maambukizi kupitia matone, akipumua au akikohoa.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...