Search This Blog

Saturday, September 18, 2021

Majokofu yanayochafua hewa marufuku



Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Selemani Jafo amepiga marufuku uingizwaji wa bidhaa zinazozalisha hewa isiyo salama kwa binadamu hasa kwa bidhaa zinazotumia gesi Zikiwemo za majokofu na viyoyozi.

Mhe. Jafo ameyabainisha hayo Jijini Dodoma kwenye ukaguzi wa maeneo ya mafundi mchundo na maeneo ambayo yanazalisha vifaa vinavyotumia gesi ambapo ameagiza wafanyabiashara na wawekezaji kuacha kujihusisha na bidhaa hizo na badala yake waweke bidhaa rafiki kwa mazingira ili kuondokana na uharibifu wa tabaka la hewa na kuendana na mabadiliko ya tabia nchi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...