Search This Blog
Friday, September 10, 2021
Gari la Marehemu Tupac Shakur lauzwa bilioni 4
Gari la Marehemu Tupac Shakur ambalo alikuwa akilitumia yapata miaka 25 iliyopita aina ya BMW 750IL la mwaka 1996 linauzwa kwa dola milioni 1.7 za Marekani ambazo ni takribani Bilioni 4 za Kitanzania.
Gari hilo ambalo alipigwa nayo risasi akiwa ndani yake usiku wa Septemba 7, mwaka 1996 na kupelekea kufariki dunia siku sita baadaye kufuatia shambulio hilo ambalo liliruhusu risasi nne kuingia mwilini mwake, akiwa na mtayarishaji Suge Knight.
Kwasasa liko kwenye eneo la maonyesho ya magari ya watu maarufu huko Las Vegas limekarabatiwa, mashimo yaliyotokana na risasi yamezibwa na kurudishwa katika hali yake mpya.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment