Search This Blog

Wednesday, September 22, 2021

Gabby Petito: Mwili uliopatikana Wyoming ni wa mwanablogu wa 'van life' aliyetoweka


Shirika la upelelezi la Marekani(FBI) limethibitisha kwamba mwili uliopatikanandani ya mbuga ya Wyoming siku ya Jumapili ni wa mwanablogu wa "van life" Gabby Petito.

Mtaalam aligundua mwanzoni kwamba kifo chake kilikuwa mauaji lakini hakutoa ishara ya jinsi alivyokufa.

Bi. Petito, 22, alikuwa akizuru mbuga ya kitaifa ya Grand Teton akiwa na mchumba wake, Brian Laundrie, 23.

Polisi kwa sasa wanamtafuta Bw.Laundrie, ambaye hajulikani aliko.

Anachukuliwa kama "mshukiwa" katika kesi, lakini hajashtakiwa kwa uhalifu wowote.

Hakuna maelezo kuhusu uchunguzi wa maiti yaliyotolewa.

Familia ya Bi Petito iliripoti kupotea kwake siku 10 baadaye.

Wiki kadhaa kabla ya hapo, polisi wa Utah mjini Moab walifahamishwa kuhusu uwezekano wa mzozo wa kinyumbani.

Kanda za Bodycam ilimuonesha Bi Petito akilia na kulalamika kuhusu hali yake afya ya akili.

Ripoti ya polisi baadaye ilisema Bw. Laundrie alidai Bi Petito alimpiga wakati wa mabishano.

Hakuna mashtaka yaliyowasilishwa, na maafisa walipendekeza kwamba wenzi hao wasilalale mahali. Kilichofanyika baadaye hakikubainika.

 




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...