Manumba alifariki Agosti 30, 2021 majira ya saa 9 alasiri katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa maradhi ya figo ambayo yalimsumbua kwa muda mrefu.
Akizungumza na Mwananchi Digital kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi mkoa wa Simiyu, Richard Abwao amesema mazishi yatafuata taratibu zote za kijeshi.
"Alikuwa kiongozi wetu wa kijeshi kwa hiyo hata mazishi yake yatafanyika kwa kufuata taratibu za kijeshi chini ya Jeshi la Polisi," amesema Abwao.
Ameongeza kwamba jeshi limeandaa utaratibu wa kuwaongoza waombolezaji watakaohudhuria katika mazishi hayo.
Manumba alijiunga na jeshi la Polisi 1976 na kulitumikia kwa miaka 37 hadi alipostaafu 2013.

No comments:
Post a Comment