
China imetuma ndege 24 za kivita kuelekea Taiwan, katika maoenesho makubwa ya nguvu leo, baada ya kisiwa hicho kinachojitawala kutangaza azma yake ya kujiunga na kanda ya kibiashara ya Pasifiki, ambayo China pia imeomba kujiunga nayo.
Jeshi la ukombozi wa Watu wa China limerusha ndege zake za kivita kuelekea Taiwan mara mbili, mara moja asubuhi kwa ndege 19, na pia mchana kwa ndege tano.
Wizara ya ulinzi ya kisiwa hicho imesema Taiwan ilipeleka vikosi vya doria ya angani kama jibu kwa ndege za China, na kuzifuatilia kwenye mifumo yake ya ulinzi.
China imekuwa ikituma ndege kuelekea Taiwan karibu kila siku katika mwaka uliyopita, na imeongeza unyanyasaji wake wa kijeshi dhidi ya kisiwa hicho, kufuatia matukio ya kisiasa ambayo inayaona kama yanaingilia mamlaka yake.
China na Taiwan zilitengana wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vya mwaka 1949, lakini China inaendelea kudai Taiwan ni sehemu ya ardhi yake, na inapinga ushiriki wa Taiwan katika mshirika ya kimataifa.
No comments:
Post a Comment