Search This Blog

Thursday, September 2, 2021

Afrika Kusini yakataa kuwa mwenyeji wa wakimbizi wa Afghanistan


Afrika Kusini imesema haiwezi kuchukua wakimbizi kutoka Afghanistan licha ya ombi.

"Afrika Kusini tayari ni makazi ya idadi kubwa ya wakimbizi na imebanwa kushughulikia mahitaji yao," Idara ya Uhusiano wa Kimataifa ilisema katika taarifa yake.

Ilisema ilikuwa imeombwa kuchukua wakimbizi ambao walikuwa nchini Pakistan kwa nchi wanazopitia.

Lakini ilisema haikuwa katika nafasi ya kukubali "wakimbizi watahudumiwa vyema kwa kubaki Pakistan, nchi yao ya kwanza ya kuwasili".

Baadhi ya nchi nyingine kama Rwanda na Uganda tayari zimekubali kuwa wenyeji wa wakimbizi wa Afghanistan wakati wanasubiri kupelekwa katika nchi nyingine.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...