Search This Blog

Sunday, September 5, 2021

Acheni kuingilia majukumu ya watu wengine


Na Maridhia Ngemela, Mwanza.

Viongozi  wa kuchaguliwa  wameshauriwa kutoingilia majukumu ya watendaji wa Serikali katika ziara zao za kutimiza wajibu wao kwani imekuwa ikifedhehesha baadhi ya watumishi wa umma.

 Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza Zebedayo Selemani alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuwa imekuwa kero kubwa kwa watendaji wa Serikali kukosa amani na uwajibikaji wao kutoka kwa baadhi ya viongozi wa siasa kuwafedhehesha mbele ya wananchi  na kuleta athari kwa jamii inayoishi nao kuwachukulia ni wakosefu wa nidhamu katika utendaji kazi wao.

"Amesema imefikia mahali sasa  wao ndio wamekuwa mahakimu,takukuru ,askari  kwenye mikutano ya hadhara akiangalia kitu anasema umeiba,wenye  mamlaka ya kukamata ni polisi tena kwa maelekezo yenye staha hii maana njia wanazotumia viongozi wa siasa unaweza ikaleta  athari kuchonganisha jamii na mtendaji wa serikali  lazima tutumie vyombo husika  nashauri tutumie vyombo ili vifanye kazi zao maana sasa Hawa watafanya kazi gani ?"amesema Zebedayo.

Ameishauri jamii kuendelea kufuata kwanini za afya ili kuendelea kujikinga na ugonjwa wa uviko 19 na kuweza kupata kinga ya chaji ambayo ni salama kwa Watanzani.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...