
Nchi ya Falme za Kiarabu (UAE) itafungua milango yake kwa watalii wote, ikiwa watapewa chanjo, kama sehemu ya hatua mpya za corona (Kovid-19).
Mamlaka ya Kitaifa ya UAE inayohusika na Majanga ya Dharura ilitoa taarifa iliyoandikwa juu ya watalii ambao wanataka kuingia nchini na visa.
Katika taarifa hiyo, ilielezwa kuwa watalii ambao wanataka kusafiri kwenda UAE watapewa visa ikiwa watachomwa chanjo, kwa uboreshaji wa uchumi wa nchi hiyo na masilahi ya afya ya umma.
Katika taarifa hiyo, ilibainika kuwa uamuzi huo utaanza kutekelezwa kuanzia Agosti 30.
Mnamo Mei, UAE ilisitisha safari zote za ndege kwenda India, Pakistan, Nepal, Sri Lanka, Uganda na Nigeria kwa sababu ya kuongezeka kwa kesi za maambukizi ya Kovid-19.
No comments:
Post a Comment