
Wakati Ndege ya Marekani inaondoka Afghanistan bado kulikuwa na raia wa Marekani na Waafghani waliokuwa wakitarajia kuondoka, wakijaribu kuingia kwenye uwanja wa ndege, maafisa wameeleza.
Katika mkutano wa waandishi wa habari awali, Jeneali McKenzie, Mkuu wa vikosi vya Marekani alithibitisha kuwa kuna Wamarekani 100-250 ambao wameshindwa kufika uwanja wa ndege au wameshindwa kuingia kwenye ndege.
Mwanajeshi wa zamani wa Marekani ambaye amesema kuwa alikuwa akisaidia kuratibu shughuli za uokoaji akiwa katika makazi yake Connectcut amesema Taliban waliwazuia wengi kupita. Alikuwa akiwasiliana na wengi, aliandika katika ukurasa wa twitter.
''Taliban walikuwa hawawezekani kuratibu nao mpaka mwiho. Walikataa kutoa ushirikiano nje ya milango ya kuingilia,'' alisema.
BBC haijathibitisha madai haya.
Alex Plitsas, Mwanajeshi wa zamani amesema bado anawasiliana na Wamarekani wanaotaka kuondoka Afghanistan, lakini baadhi hawajajisajili kwenye mamlaka za Marekani ''Hatuwezi kuwaokoa watu ambao hatujui kama wako huko,'' alisema.
No comments:
Post a Comment