Kulingana na diwani Raz Mohammad na wabunge wawili wanaoliwakilisha jimbo hilo, kundi hilo la waasi limeteka vituo vikuu vya serikali katika mji wa Aybak ambao ni mji mkuu wa jimbo la Samangan. Vikosi vinavyoiunga mkono serikali viliuacha mji huo na kukimbilia kwenye kilima cha Koh-e Bast baada ya serikali kuu kushindwa kupeleka nyongeza ya askari na haikutekeleza mashambulizi ya angani kuvisaidia vikosi vya serikali.
Hata hivyo mbunge mwingine kutoka kwenye eneo bunge hilo amesema askari wengine wapya 300 watapelekwa ili kusaidia operesheni ya kuwashinikiza Taliban kuondoka kutoka kwne mji wa Aybak, wenye wakazi zaidi ya 120,000.
Hapo jana wanamgambo wa Taliban waliiteka miji mikuu mitatu ya Kunduz, Sar-e Pul na Taluqan. Wapiganaji wa Taliban wamechukua zaidi ya nusu ya wilaya za Afghanistan wakati ambapo majeshi ya Marekani na NATO yanakamilisha hatua za kuondoka kabisa nchini humo.

No comments:
Post a Comment