Kikosi cha Ulinzi cha Rwanda (RDF) kimeanza shughuli ya kuwapeleka wanajeshi 750 wa kujiunga na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINUSCA), kulingana na taarifa kutoka kwa jeshi.
Kundi la kwanza la walinda amani 300 wakiongozwa na Luteni Kanali Patrick Rugomboka kiliondoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kigali kuelekea Bangui, Jumanne.
Walipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Bangui, walinda amani wa Rwanda walikaribishwa na Kamanda wa Kikosi cha MINUSCA, Luteni Jenerali SADIKI Traoré akifuatana na Mkuu wa Wafanyikazi wa Kikosi cha Wanajeshi wa Jamuhuri ya Afrika ya Kati, Jenerali Zephlin Mamadou.
Kamanda wa Kikosi alitoa shukrani zake kwa walinda amani wa Rwanda kwa kujitolea kwao bila kutetereka kulinda raia na kudumisha amani na usalama huko CAR.
Kulingana na RDF, kikosi hicho kitapewa jukumu ulinzi katika njia kuu ya usambazaji (MSR1) inayounganisha Bangui na mpaka na Cameroon.
Kufuatia hatua hii Rwanda sasa itakuwa na vikosi vitatu pamoja na Hospitali ya kiwango cha pili iliyowekwa chini ya MINUSCA.

No comments:
Post a Comment