Rais mpya wa Zambia Hakainde Hichilema amewaondoa makamanda wakuu wa jeshi la nchi hiyo na mkuu wa polisi - na kuashiria mwelekeo wa vikosi vya usalama kuwajibika zaidi kwa raia.
Jumapili Rais Hichilema alitangaza makamanda wapya wa jeshi la Zambia, jeshi la anga na huduma ya kitaifa na manaibu wao, na vile vile inspekta jenerali mpya wa polisi.
Makamishna wote wa polisi wa mkoa wameondolewa majukumu yao lakini nafasi zao hazijajazwa.
Bwana Hichilema alisema viongozi wapya wa ofisi "lazima wawe kwa maslahi ya watu kwa moyo na watumikie nchi kwa bidii wakati wanahakikisha haki za binadamu, uhuru na uhuru vinaheshimiwa," alisema.
Alisema polisi lazima wafanye uchunguzi sahihi kabla ya kuwakamata washukiwa na kwamba "hakuna mtu anayepaswa kukamatwa kabla ya uchunguzi kukamilika".
Bwana Hakainde, ambaye alichaguliwa kuwa rais mapema mwezi huu kwa ushindi wa kishindo, amekuwa mwathirika wa ukatili wa polisi hapo zamani.
Alikamatwa na kuzuiwa mara kadhaa huko nyuma - na alikuwa ameahidi kushughulika na unyanyasaji wa vikosi vya usalama.
No comments:
Post a Comment