Search This Blog

Saturday, August 28, 2021

Rais wa zamani wa mpito wa Mali aondolewa katika kizuizi cha nyumbani


Jumuiya ya Kiuchumi ya Mataifa ya Afrika Magharibi - ECOWAS imesema rais wa zamani wa mpito wa Mali, Bah Ndaw na waziri mkuu wake Moctar Ouane wameondolea katika kizuizi cha nyumbani.
 
Katika taarifa hiyo ya ECOWAS inaikaribisha hatua hiyo ya Mali, ya kuowaondolea vizuizi viongozi wote wa zamani na kusema viongozi wote hao wawili wanapaswa kupata fursa na haki zote za kimsingi kama rais wa zamani na waziri mkuu wa zamani.
 
Kabla ya kuondolewa madarakani katika mapinduzi ya pili na Kanali Assimi Goita, rais huyo wa zamani wa mpito wa Mali, Bah Ndaw na waziri mkuu wake Moctar Ouane walichaguliwa kama viongozi wa kiraia baada ya mapinduzi ya kijeshi ya Agosti 2020.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...