Katika mazungumzo yake ya kwanza ya simu na kiongozi wa Magharibi, Raisi, aliye na msimamo mkali na ambaye alichukua madaraka wiki iliyopita, alimwambia Macron kuwa Marekani na Umoja wa Ulaya lazima zitekeleze ahadi zao chini ya muafaka wa kihistoria wa 2015.
Ufaransa, pamoja na Marekani, Ujerumani, Uingereza, Urusi na China ilikuwa sehemu ya makubaliano ya awali ya nyuklia mnamo mwaka wa 2015 na imekuwa na jukumu kubwa kama mpatanishi.
Rais amesema katika mazungumzo yoyote, haki za taifa la Iran zinapaswa kulindwa, huku akiikosoa Marekani kwa kujiondoa katika makubaliano hayo na kutangaza vikwazo vipya chini ya Rais wa zamani Donald Trump.

No comments:
Post a Comment