Search This Blog

Thursday, August 19, 2021

Mafuriko yasababisha vifo nchini Ethiopia


Kulingana na ripoti za awali, watu 7 walifariki katika mafuriko yaliyotokea huko Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia.

Katika taarifa iliyotolewa na Timu ya Zimamoto, Kinga ya Dharura na Uokoaji huko Addis Ababa, iliripotiwa kuwa mvua kubwa iliyonyesha ghafla jana jioni ilisababisha mafuriko.

Taarifa zaidi iliarifu kwamba watu 7 walipoteza maisha na wengine wengi walijeruhiwa kutokana na mafuriko hayo.

Juhudi za utafutaji na uokoaji zimeanzishwa kwa wale waliopotea kwenye mafuriko, ambapo nyumba nyingi ziliharibiwa.

 




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...