Search This Blog

Monday, August 2, 2021

Madagascar yawakamata majenerali waliopanga kumuua Rais Rajoelina

Maafisa wa kijeshi wa ngazi ya juu na polisi wamekamatwa nchini Madagascar kuhusiana na jaribio la kumuua rais lililotibuka.

Waliokamatwa ni pamoja na majenerali watano na maafisa kadhaa wa polisi na kufikisha 21 jumla ya watu ambao wanachunguzwa ufuatia tukio hilo a mwezi uliopita.

Mamlaka pia imepata bunduki moja na dola 250,000 za Kimarekani, vyombo vya habari nchini humo vimeripoti.

Jaribio la kumuua Rais Andry Rajoelina ni sehemu ya misukosoko ambayo imekuwa ikikumba taifa hilo la kisiwani.

Madagascar imekuwa ikitekeleza amri ya kutotoka nje tangu janga la Covid-19 lilipozuka mwaka jana huku sehemu ya kusini mwa nchi hiyo ikikabiliwa na hatari ya kukumbwa na baa la njaa.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...