Search This Blog

Thursday, August 5, 2021

Maambukizi ya covid-19 yaongezeka Iran

Kesi za maambukizi ya virusi vya corona (Kovid-19), ambazo zilipungua nchini Iran mwanzoni mwa Juni, zilipanda hadi viwango vya rekodi kutokana na kasi ndogo ya chanjo na umma kutofuata sheria kama uvaaji barakoa na kuzingatia umbali wa kijamii.

Nchini Iran, ambapo mchakato wa chanjo ulianza mnamo Februari 9 kwa kujumuisha Sinopharm, Sputnik V na AstraZeneca pamoja na chanjo ya ndani ya COVIRAN Bereket, imekuwa ikitumika tangu Juni 25, baada ya matumizi ya dharura kuruhusiwa mnamo Juni 14.

Jumla ya dozi milioni 13.5 za chanjo zimetumiwa hadi sasa kati ya idadi ya watu takriban milioni 83, na wimbi la 5 limetokea tangu Julai wakati kesi zilifikia viwango vya rekodi, na idadi kubwa ya vifo vya kila siku  iliyokuwa imepungua hadi 100, iliongezeka tena hadi zaidi ya 400.

Ili kudhibiti kesi za maambukizi zinazoongezeka, serikali ilitangaza likizo ya siku 6 baada ya sikukuu na kuharakisha mchakato wa chanjo.

Idadi ya vifo vya kila siku nchini, ambayo ilipungua hadi 100 mnamo 7 Juni, iliongezeka hadi 411 mnamo Agosti 2. Idadi ya kesi za maambukizi ya kila siku, ambazo zilipungua hadi 4,907, zilirekodiwa kama 39,019 hapo jana.

Wakati inasemekana kuwa hospitali katika majimbo mengi zimejaa kikamilifu, inadaiwa kwamba hakuna nafasi katika makaburi kwa sababu ya kuongezeka kwa vifo. Imeripotiwa kuwa Bodi ya Kitaifa ya Kupambana na Corona, ambayo imepanga kuongeza hatua hizo, inaweza kuchukua uamuzi wa vizuizi vya wiki 2 katika mji mkuu Tehran.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...