Ditopile ameuliza swali hilo leo Bungeni wakati wa kipindi cha Maswali na Majibu ambapo Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema tayari Serikali ishaingia mkataba na wasambazaji wa mbegu kwa ajili ya kusambaza mbegu bora za zao hilo.
" Niipongeze sana Serikali yetu kwa muda mfupi tu imeweza kupandisha thamani ya Zao la Alizeti ambapo bei imepanda hadi Sh 1600 kwa Kilo Moja, hii haijawahi kutokea kwenye Nchi yetu, kupanda huku kwa bei kumesababisha muamko uwe mkubwa kwa watu kwenda kulima Alizeti, Je Serikali imejipangaje kuhakikisha inawezesha upatikanaji wa mbegu bora kwa ajili ya msimu mpya wa Kilimo hasa kwa wakulima wetu wa Dodoma,"?
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema kwa sasa Serikali imeanza kuchukua mahitaji ya Mikoa wanayoleta wenyewe kutokana na uwezo wa Mkoa husika katika suala la uzalishaji ambapo katika Mkoa wa Dodoma wanashirikiana kwa karibu na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kupitia Katibu Tawala wa Mkoa.
" Kwa sasa tunashirikiana na Ofisi ya RAS kutuletea mahitaji ya Wilaya zote ili sisi kama Wizara tuweze kuwapatia mbegu, nataka niwahakikishie wakulima tutahakikisha wakulima wa Alizeti wanapata mbegu bora ambazo zitaweza kuwasaidia mwaka huu wakati ambao sisi Serikali tunajipanga kwa mwaka mwingine," Amesema Bashe.
Search This Blog
Tuesday, August 31, 2021
Ditopile aiomba Serikali kuwezesha upatikanaji wa Mbegu Bora za Alizeti
MBUNGE wa Viti Maalum Wanawake Mkoa wa Dodoma, Mariam Ditopile ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa kuwezesha bei ya zao la Alizeti kupanda hadi Sh 1600 kwa Kilo Moja lakini akaihoji Serikali imejipangaje kuwawezesha wakulima wa zao hilo kupata mbegu bora na za kisasa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment