Search This Blog

Tuesday, August 10, 2021

Bahasha yenye risasi tatu ndani yatumwa kwa Papa Francis


Bahasha iliyo na risasi 3 ilitumwa kwa kiongozi wa kiroho wa Wakatoliki Papa Francis.

Risasi 3 za milimita 9 na ujumbe juu ya shughuli za kifedha huko Vatican zilipatikana ndani ya bahasha hiyo iliyofika ofisi ya posta karibu na Milan nchini Italia.

Wafanyakazi wa posta ambao walipata bahasha iliyotumwa kwa Papa Francis mara moja waliwaarifu polisi.

Maafisa wa polisi walichukuwa bahasha hiyo na kuanzisha uchunguzi juu ya tukio hilo.

Ilitangazwa kuwa bahasha ilitumwa kutoka Ufaransa na anwani "Papa, Jiji la Vatican, Mraba wa Mtakatifu Petro, Roma" ziliandikwa juu yake.

Hadi kufikia sasa bado hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na Vatican.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...