Bahasha iliyo na risasi 3 ilitumwa kwa kiongozi wa kiroho wa Wakatoliki Papa Francis.
Risasi 3 za milimita 9 na ujumbe juu ya shughuli za kifedha huko Vatican zilipatikana ndani ya bahasha hiyo iliyofika ofisi ya posta karibu na Milan nchini Italia.
Wafanyakazi wa posta ambao walipata bahasha iliyotumwa kwa Papa Francis mara moja waliwaarifu polisi.
Maafisa wa polisi walichukuwa bahasha hiyo na kuanzisha uchunguzi juu ya tukio hilo.
Ilitangazwa kuwa bahasha ilitumwa kutoka Ufaransa na anwani "Papa, Jiji la Vatican, Mraba wa Mtakatifu Petro, Roma" ziliandikwa juu yake.
Hadi kufikia sasa bado hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na Vatican.

No comments:
Post a Comment