Search This Blog

Thursday, August 12, 2021

Afisa wa huduma ya afya afanyiwa uchunguzi kwa kuchoma maelfu ya watu maji ya chumvi badala ya chanjo nchini Ujerumani

Afisa mmoja anayefanya kazi katika kituo cha chanjo cha Schortens cha mkoa wa Friesland wa Lower Saxony, Ujerumani, aliitumia mchanganyiko wa maji ya chumvi badala ya chanjo ya corona (Kovid-19) kwa maelfu ya watu.

Gavana wa Friesland Sven Ambrosy alisema kuwa mnamo Machi na Aprili, ingawa hakuwa na hakika idadi kamili, takriban watu 9,650 walipewa maji ya chumvi badala ya chanjo za Biontech, Moderna na Astrazeneca.

Ilipogundulika kuwa afisa wa huduma ya afya aliingiza mchanganyiko wa maji ya chumvi badala ya chanjo ya Kovid-19, wale waliokuwa wamekumbwa na hali hiyo kati ya Machi 5 na Aprili 21 waliitwa kuchomwa chanjo tena.

Ilibainika kuwa ofisi ya mwendesha mashtaka inaendelea kuchunguza suala hilo.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...